Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania, umeeleza kufurahishwa na hatua ya kushirikishwa kwa nyota Diamond Platnumz kwenye album mpya ya Alicia Keys, ‘ALICIA’.

Kupitia mtandao wa twitter wa Ubalozi huo, ulieleza kuwa ni furaha yao kuona Alicia Keys wa nchini Marekani kumshirikisha Diamond kutoka Tanzania kwenye wimbo ‘Wasted Energy’ kwenye album hiyo.

Hata hivyo Ujumbe huo wa Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania uliombatana na link ya wimbo huo wa kutoka kwenye Mtandao wa Youtube, uliutaja wimbo huo kuwa ni wimbo wa moto.
Ujumbe wa Ubalozi huo kwenye Ukurasa wa Twitter
Inafurahisha kuona msanii @aliciakeys akimshirikisha msanii wa Kitanzania, @diamondplatnmz
Goma jipya la #WastedEnergy ni🔥🔥
—
Great to see American artist @aliciakeys collaborate w/Tanzanian artist @DiamondPlatnumz.New track #WastedEnergy is 🔥🔥 https://t.co/RV0z1sSOwl
— US Embassy Tanzania (@usembassytz) September 20, 2020
Usikilizew eimbo huo hapa chini.